Wednesday, April 23, 2014

MSTARI WA KIZUSHI: NI KILA JUMATANO MKALI WANGU.

Yaap, kama kawa mwanangu mwenyewe yaani kama nakuona vile ilivyoitolea jicho safu hii kwa ijumaa hii tulivu, ila itakuwa mwake kiaina kama baada ya kuusoma ukurasa huu ukalihifadhi gazeti lako ili siku ya siku ujikumbushe kwa mara nyingine na kupitia mawili matatu, ila haiko poa kama Dadangu pale uswazi mtoto haja kuu halafu wewe ukazolea ile kitu, sio swala la kucheka sasa!


Oya, gwala kwa masela tulio kisongesha pamoko juzi ile kwenye ka ukurasa haka na iko poa zaidi kwa wale mliotoa ushauri kupongeza na mliouliza maswali na nikawajibu na kuwafafanulia kinaga ubaga kulingana na maswali mliyo yauliza ila sina maana ya kwamba muendeleze maswali, mwisho wa maswali ni ile juzi kati ok?
Tusonge sasa Mwana wane,
Katika meseji mbali mbali zinazosambazwa kupitia simu za mkononi kuna moja kali sana, hii inawazungumzia wa Bongo na uvivu, tena hadi kwenye mambo muhimu.

 Kwa mujibu wa mtunzi wa meseji hiyo ni kwamba wabongo kadhaa walivamia Benki kwa minajili ya kukomba mkwanja ambapo dhamira yao hiyo ilifanikiwa kwa kiasi kinene na baada ya kukomba miburungutu wakafikanayo  mafichoni wakiwa salama, lakini walipofika mafichoni mmoja kati yao akawaambia wenzake.

 “Oya, hela hizi nyingi mno ka’ vipi nyie endeleeni kuzihesabu mtaniambia kesho ziko shingapi.”
Umeicheki hii, kama hauja nisoma mwishoni utanisoma mwana, iko hivi,
Mwishoni mwa miaka ya 90 bongo flavor ilikuwa juu sana kiasi kwamba baadhi ya wasanii kama Profesa Jay,  Juma nature na wengineo wengi nyimbo zao zilikuwa ni mfano wa nyimbo za taifa kwa jinsi zilivyokuwa zikipendwa mitaani na popote ambapo zingesikika,  ikiwa Profesa Jay  alikuwa na wimbo mpya basi kila kona ya jiji ungesikia watu wakisimuliana “Bwana umeisikia Ndiyo mzee, ni balaa.” Hata hivyo hali hii ikaja kuzoeleka baada ya miaka kadhaa na baadaye ikaanza kuonekana ni ya kawaida tu.

Lakini miaka ya 2000 akaibuka msanii Mjomba mpoto, huyu mkali ingawa alikuwa na ngoma mbili tatu kabla lakini ngoma iliyomuweka pazuri ilikuwa ni ngoma iliyosonga kwa jina la  ‘MJOMBA’  kuanzia mistari ya ngoma hii biti na hadi staili yenyewe ya uimbaji ikaitikisa nchi Serikali na raia wake, huyu jamaa aliingia na staili kughani mashairi yake kwa kuongea  ikapokelewa kwa mikono yote miwili.
Mchekeshaji maarufu hapa nchini wa kundi la Orijino Comedi Mpoki alikuwa mfano wa wale wabongo niliowataja  pale juu ( wavivu ) hakutaka kuumiza kichwa badala ya kubuni staili na mbinu za kuiteka jamii ya wapenda muziki yeye akaugeuza tu ule wimbo wa Mpoto, wake akauita  ‘SHANGAZI’  lakini kila kitu akafanya kama alivyofanya Mpoto hata hivyo hili halikuwashangaza wengi kwani ni wengi tu wametoka kwa staili za kukopi.

Mwaka uliofuata baada ya mpoki kukopi wimbo ule wa Mpoto kulikuwa na tuzo za Kilimanjaro na katika wasanii waliokuwa wakigombea tuzo ya muziki wa asili wawili hao ndiyo walikuwemo Mpoki kupitia wimbo wa Shangazi na Mpoto kupitia Adela lakini hata hivyo Mpoki akaibuka kidedea na kunyakua tuzo hiyo.
Baada ya kupokea tuzo hiyo akasema “HATA JOGOO ANAWAHI KUAMKA LAKINI HAWEZI KUFUNGUA MLANGO.”  Kwa utashi wangu ni kwamba kijembe hicho alikuwa akipigwa Mpoto kwamba  ni wa kwanza kubuni  staili ya kuongea lakini ameshindwa kupewa tuzo.
Kuna nilichobakiza? 

Sasa, minasepa wanangu wenyewe hadi wiki nyingine, Adios!

No comments:

Post a Comment

KATUNI ZA MWAGITO HIZI HAPA MWANANGU.