Wednesday, September 17, 2014

HADITHI YA POLENI WAPIGA KURA-ISOME HAPA

POLENI WAPIGA KURA

Mpenzi msomaji samahani kwa kukucheleweshea hadithi hii kutokana na tatizo la umeme ofisini kwetu lakini naahidi kuwa juimatano ijayo itawahi.   Mwandishi.

Imeandikwa na Shedrack Kilasi

Sithubutu na sito thubutu kufanya ujinga huo, sitaki nipige halafu kesho na kesho kutwa nitamani mtu niliyempigia afe au aondolewe madarakani kutokana na uzembe wake wa kuto waletea maendeleo watu na kujinufaisha yeye mwenyewe kwa lasilimali za jamii husika kwani kumlaumu au kutaka lolote baya limpate ili aachie ngazi itakuwa ni dhambi kwangu.
Nidhambi kuu pia kuwaacha wanangu wakikingojea kitumbua cha kila siku halafu mimi nikaenda kupanga foleni kutwa nzima nikingojea kumpigia kura mtu ambaye ataisaliti nchi yangu, atalisafisha jiji pindi tu atakapokuja rais wa nchi kubwa ya Magharibi lakini baada ya siku kadhaa jiji litaendelea kunuka na wananchi wake wa hali ya chini kufanya biashara hovyo kwenye vituo vya mabasi na sehemu nyingine hatarishi.
Yap, dunia na taifa wanajua kwamba naichukia Siasa, hii siasa ndiyo iliyomfanya Bibi na babu yangu wakafa bila kumsomesha mama yangu, ni siasa hiyo hiyo iliyomfanya mama yangu akashindwa kuntusomesha na badala yake akajiingiza kumshabikia mwanasiasa wa jimboni mwake na kumpigania mpaka akapata Ubunge na kisha baadaye akawa Spika wa Bunge lakini siku ya kumsiba wake hatukumuona na mbaya zaidi hakufanya lolote siku serikali ilipoamua kuudhulumu ukoo wetu maeneo ya viwanja yaliyopo jimboni humo.

Lakini pia siipendi  Siasa kwakuwa inapingana na ukweli na nawachukia waumini wake kwakuwa wameshawadanganya mno ndugu zangu wajinga, wakati mwingine na kaa na washkaji maskani  lakini wakianza kuongelea mambo ya kuwasifia baadhi ya watu wa chama fulani naamua kuondoka zangu kwani naamini hakuna cha afadhali, na ninasisitiza kwa chochote unachokifanya ukipata nafasi ya kula kula tu ndugu yangu kwani kuna watu wanakula zaidi ya mnavyotegemea.
Huu ni ujumbe na ni maoni yangu tu sikulazimishi uamini vile ninayoamini mimi ila mwisho wa siku nakushauri fanya mambo yako achana na mambo ya siasa!

DIBAJI.
Ni miaka 20 tangu alipofariki mama yangu mzazi na tangu hapo ndipo nilipoanza kuichukia siasa lakini kwakuwa nilikuwa mdogo nikataka kupambana hadi mwisho ili kujua ni jinsi gani taifa langu linaangamia kwa uozo huu wa viongozi wachache, haikuwa rahisi na kwa mawazo ya watoto wengi wa enzi zangu naamini mimi nilikuwa ni gwiji kwakuwa juhudi zangu zilinifungua zaidi ya msomi wa pale mlimani.
Kitu cha kwanza nilifikili kujiingiza kwenye vyombo vya habari kwakuwa vyenyewe ndivyo vilivyokuwa vikiripoti matukio mengi ya siasa ulaji rushwa na ufisadi, nikagundua pia kuwa wengi wa wanasiasa wenyewe hutokea huku huku hili likaniaminisha kuwa ndani ya miaka 20 au zaidi nitakuwa na kitu cha kuipa jamii…pakoje?   Songa nayo sasa!
Yap, kimya kimya mithili ya mtu akimbizaye mwizi baada ya kufanya kazi kwenye vyombo vya habari kwa miaka 20 nikaachana nayo kwani  ingawa ilikuwa hainilipi mimi nilikuwa nikifanya uchunguzi wangu binafsi, ingawa kwenye ofisi niliyokuwa nikifanya kazi watu walionizunguka walikuwa wamenizowea kupita kiasi lakini niliamua kuipiga teke kazi hii ili kuelekea kulikomboa taifa langu masikini hivyo kwakuwa nilikuwa na vyeti vinavyokubalika vya shule nikaamua kuingia jeshini ambapo baada ya kukubaliwa nilijiunga  na jeshi na ndani ya miaka miwili nikaonekana ninakipaji cha kipekee na juhudio kazini hivyo nikaulizwa kama nilihitaji kusomea ukomando kitu ambacho nilikuwa nikikiwaza tangu siku naingia jeshini hivyo hata siku na kipingamizi ikawa hivyo.

Miaka sita ilitosha mimi kukaa Urusi na baada ya kurudi nchini Razam nilikuwa chimbo wakati huu wote mambo ya kishenzi yalikuwa yakiendelea kutokea nchini mwangu ikiwa ni pamoja na ufisadi kuuawa kwa watu wanaouliza ukweli au kuwa na uhakika wa kigogo aliyekula rushwa sanjali na wakubwa kuruhusu meli za kuchimba mafuta kuingia nchini kinyemela huku wanachi wakiamini ni mafuta ya Sample yaliyokuwa yakichukuliwa na meli hizo kubwa kila leo.

No comments:

Post a Comment

KATUNI ZA MWAGITO HIZI HAPA MWANANGU.