Timu ya Mari Fc. Inayoundwa na kituo cha utafiti wa kilimo
Mikocheni mwishoni mwa wiki ilikubali kipigo cha mabao mawili kwa nunge kutoka
kwa timu ngumu ya Changanyikeni Veterani kwenye mtanange wa kirafiki uliopigwa
kwenye nyasi za uwanja wa chuo cha Takwimu kilichopo maeneo ya Changanyikeni.
Iliwachukua dakika 30 pekee Changanyikeni kuandika bao la
kwanza kupitia kwa Adam Mshamu ambaye alifunga bao hilo kwa njia ya penati
baada ya beki wa timu ya Mari Fc Dk. Joseph Mdugara kuunawa mpira ndani ya eneo
la hatari na mwamuzi Kasonta kuamuru lipigwe tuta.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku kila timu ikifanya
mabadiliko ingawa mabadiliko hayo yaliinufaisha zaidi timu ya Changanyikeni
Veterani ambapo kunako dakika ya 41 winga wa timu hiyo alipiga krosi safi
iliyomkuta beki wa Mari Fc. Mwelam Mohamed na kuutumbukiza mpira kimiani wakati
akijitahidi kuokoa.
Kocha wa Mari Fc.Zakaria Muyuyi Alisema vijana wake
walijitahidi ingawa walizidiwa kidogo mbinu za kiuchezaji na wachezaji wa timu pinzani lakini hata
hivyo akasema kipigo hicho kimewapa changamoto kabla ya ziara yao ambayo
inatarajiwa kufanyika mwezi ujao mjini Zanzibar.
Naye mzee wa timu hiyo Said Minazi Komba alisema timu hiyo
ambayo inaongozwa na Dk.Joseph Mdugara licha ya ziara hiyo ya Zanzibar pia
inajiandaa na mechi kadhaa za kimataifa ambazo zitapigwa nchini na nje ya nchi.
No comments:
Post a Comment