Timu ya soka ya Mari Fc.
Inayoundwa na wafanyakazi wa kituo cha utafiti wa kilimo kilichopo maeneo ya
Mikocheni jana ilikubali kipigo cha mabao 3-2 kutoka kwa mashabiki wa yanga
waliopo kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook katika mtanange wa kirafiki
uliopigwa kwenye uwanja wa chuo cha Takwimu kilichopo maeneo ya Changanyikeni
jijini Dar.
Mashabiki hao wa wana
Jangwani ndiyo walikuwa wa kwanza kuandika bao kunako dakika ya 20 ya mchezo
kupitia kwa mshambuliaji wao Jumanne juma ambaye aliwahadaa mabeki wawili wa
timu ya Mari kabla ya kumlamba chenga na mlinda mlango wao na kisha kupachika
bao kirahisi.
Dakika tatu baadaye
Yanga walipata bao la pili kupitia kwa mshambuliaji wao hatari Yule Yule Jumanne
ambapo alipokea pasi safi kutoka wingi ya kushoto na kuukwamisha mpira ule
kimiani kiurahisi huku akimwacha kipa wa Mari Fc akiwa hana la kufanya hivyo
mpaka wanakwenda mapumziko Mari ilikuwa nyuma kwa mabao mawili kwa nunge.
Kipindi cha pili
kilianza kwa kasi huku kila timu ikifanya mabadiliko lakini almanusura
mabadiliko hayo yawe na faida kwa mali ambao walifanikiwa kusawazisha mabao
yote mawili kupitia kwa mshambuliaji wao Zacharia Muyengi lakini hata hivyo udhaifu wa mwamuzi wa mchezo huo Said Komba
Minazi uliwafanya Yanga wapate bao la tatu na matokeo kuwa 3-2.
Minazi alitoa adhabu ya
penati kutokana na mchezaji wa Yanga kukwatuliwa nje ya eneo la hatari kitu
kilicho lalamikiwa mno na wachezaji wa Mari ingawa yote kwa yote refa alibaki
kuwa mwamuzi wa mwisho na matokeo yakabaki hivyo mpaka dakika ya mwisho.
Akiongea na blog hii
mmoja wa viongozi wa Mari Zacharia Muyengi alisema mechi
hiyo imewapa changamoto na watayafanyia kazi makosa waliyoyaona ili
mechi nyingine waweze kutoka kifua mbele.
“Nashukuru kwamba kocha
viongozi wa timu na mzee wa timu kila mmoja ameyaona makosa yapo wapi hivyo
tunajipanga kuyarekebisha ili mechi zijazo tuweze kushinda kwani hizi ni mechi
za kirafiki kabla ya ile ziara yetu ya Zanzibar.” Alisema Muyengi.
No comments:
Post a Comment