Thursday, April 6, 2017

NDANI YA KIBANDAUMIZA WIKI HII



NDANI YA MABATINI STADIUM:

Kibaka asepa na mabovu ya inchaji


“AYAAAA, yule mchizi aliyekuwa amechili benchi lile yupo wapi?” Waswazi kimya huku wengine wakijitahidi kuvuta kumbukumbu za huyo anayeuliziwa bila mafanikio.
“Ebwana eeh, kazi ya kutambua watu wanaoingia humu na kutoka ni ya kwako, kazi yetu sisi ni kukulipa kiingilio na kuangalia ndiki inavyopigika,” akajibu mswazi mmoja lakini huku jicho lake likiwa tisti kunako runinga.
“Oya, masela kuweni na busara basi mjue mchizi kasepa na mabovu yote niliyoyaacha hapa,” alisema Peter.
Mwana huyo ambaye ni inchaji wa kibandaumiza kile na kuwafanya waswazi wote waliokuwa ndani humo wamgeukie kwa mshangao na jicho la huruma unajua ilikuwaje?
Wakati waswazi wakiwa wanafuatilia mbugi kideoni mara nje zikasikika kelele za mwizi, waswazi wote kibandani wakatoka mbio lakini wakati wengine wakiishia mlangoni na kurudi ndani.
 Wenzao wengine waliunga kumkimbiza kibaka akiwamo inchaji wa sehemu ile ambaye alikuwa kati ya wale waliokuwa na hamu ya kumkamata mwizi.
Kumbe inchaji huyu wakati akikurupuka na kuanza kukimbiza mwizi alikiacha kikoba chake ambacho kilikuwa na mabovu aliyotoka kuwachanja waswazi muda mfupi.
Wakati yupo kwenye purukushani hizo  ndipo mmoja wa washkaji waliokuwa karibu na kikoba hicho alipoamua kujisevia na kusepa zake kimya kimya.
Kwa mujibu wa Peter, kiasi kilichokuwa kikobani ni shilingi 57,000 ambazo alikuwa amekusanya kutoka kwa waswazi waliokuwa wakifuatilia ndiki ya Kagera dhidi ya Mnyama ambayo ilimalizika kwa matokeo kama mlivyoona na kusikia.
Ebwana eeh, hii ngoma ilikuwa ni ndani ya Mabatini Stadium, hapa naizungumzia mitaa ya Vingunguti, anasimama Joseph Martin kama mmiliki wa kibanda hiki.
Lakini Peter Muro ndiye inchaji mchanjaji wakati wote ikipigwa ndiki kubwa na hata ndogo kama hizi bwana mkubwa huyu anasimama langoni kuwachanja.
Hapa mwanakwetu wanazama waswazi 65 pekee kwa ndiki za kawaida, lakini siku kikinuka kweli kweli waswazi wanabanana na kufikia 70 ingawa siku nyingine kikinuka zaidi hufikia hadi 75 ingawa hukaa hadi kwa kubebana.
Kwa mujibu wa inchaji huku pia kuna wakishua ingawa waswazi ni wengi zaidi, wakishua wa huku siku hizi wanaachana na runinga za homu na kujichanganya uswazi kupata burudani zinazotokea ndani ya vibandaumiza na hasa siku zinapopigwa ndiki za majuu.
Buku pekee inatosha kukufanya uone ndiki ndani ya Mabatini lakini pia unaweza kuagiza kinywaji chochote au fegi ingawa si ruhusa kuvuta fegi wakati ndiki ikiendelea.
Pande hizi waswazi wanafuatilia zaidi ligi ya England ikifuatiwa na hii ya madafu ambayo hakukuwa na haja ya kuwa na ratiba.

Maana ligi hii kila uchwao hubadilika hata kwa jambo lisilo la lazima, ilimradi kinachosimamisha kiwe kinahusu mabovu, ha ha ha haaaa!!!..hii si ya humu lakini imeingia bahati mbaya tu.
Angalau waswazi wa huku nao wanaanza kupenda ligi ya Ubelgiji na wanasema mbali na Mbwana Samatta kuwa anacheza huko, lakini kinachowavutia zaidi wanandinga wa huku ni jinsi anavyozidi kupachika mabao kila uchwao na kuipeperusha bendera ya nyumbani vyema.
Hata hivyo, unaambiwa ukitoa runinga siku inapopigwa ndiki yoyote ya Italia utaishia kuhesabu viti hata iwe ni ndiki ya upinzani kiasi gani waswazi hawatoi hela.
Yaani ni bora uwawekee muvi walipie hata jero lakini si mechi labda kidogo kwa wazee wa kubeti ndio wanaweza kuangalia ili kuhakiki mikeka yao.
Ebwanaeeh, hii ni kutoka ndani ya Vingunguti kwenye Kibandaumiza cha Mabatini, mimi na wewe mkali wangu wa nguvu tugumiane kiswazi kipandeni hapa wiki ijayo lakini usikose kunialika wikiendi hii kibandani kwako.


 


No comments:

Post a Comment

KATUNI ZA MWAGITO HIZI HAPA MWANANGU.