Monday, July 21, 2014

HADITHI KILA JUMATATU


NIMESHIRIKI TENDO LA NDOA NA MAMA YANGU MZAZI KISA UTAJIRI
           
Upepo mwanana ukiwa ulivuma huku ukiambatana na milio ya Kunguru  pamoja na Jogoo kuashilia  kuwa kumekucha, ilikuwa yapata  saa 12:30 asubuhi.  kila  mtu akijiandaa kuelekea kwenye shughuli za ujenzi wa taifa. Ilikuwa ni nyumbani kwa Mzee Lumbashi maeneo ya Mbezi Kimara  mtaa wa Kinondo jijini Dar es salaam,  Mzee Lumbashi alikuwa ni mjumbe wa serikali za mtaa ambapo  kulikuwa na umati mkubwa wa watu uliotawaliwa na huzuni kubwa ya  msiba wa Mzee Lumbashi  aliyefariki dunia jana usiku katika hospitali ya taifa ya Muhimbili, Mzee Lumbashi  alikuwa akisumbuliwa na tatizo la Kisukari kwa muda mrefu. Umati huu ulikuwa ukisubiri mwili wa marehemu ambao ulikuwa bado upo kwenye chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Muhimbili. Mnamo  Saa 7:00 mchana mwili wa Mzee Lumbasi  uliwasili  na baadaye ulipumzishwa katika makaburi ya Kinondoni. Marehemu Mzee Lumbashi aliacha mke na mtoto mmoja ambaye aliitwa Hamady. Hamady na  mama yake walihuzunika sana kwa kumpoteza mtu muhimu katika familia yao aliyekuwa akitegemewa sana kwani alikuwa ni msaada mkubwa kwao,  baada ya mazishi kila mhusika aliaga kwa wafiwa na kurudi majumbani  mwao kuendelea na shughuli nyingine. Hivyo pale nyumbani walibakia Hamady  na mama yake. Haikuwa rahisi kwa usiku ule kwa hamady kupata usinginzi.
Hamady alionekana mwenye mawazo sana akifikiria majukumu atakayokuwa nayo maana alikuwa ni mtoto wa pekee  kwa marehemu Mzee Lumbashi, hivyo hakukuwa na mtu mwingine katika familia wa kuweza kusaidia familia yao.  Aliendelea kuwaza kwa muda mpaka hapo usingizi ulipompitia  na kuweza kulala.

            Ilikuwa yapata wiki moja sasa toka kuondokewa na  baba yake, haikuwa rahisi kwa Hamady kuendelea kuomboleza kutokana na majukumu ya kutunza familia yaliyokuwa yanamkabili. Hivyo aliamua kurudi tena kijiweni kwake Kariakoo kuungana na jamaa zake kuendelea na shughuli zake za ukuli, Hamady alikuwa ni mtu mwenye bidii sana ya kazi  na siku zote hakukubali kushindwa siku  zote katika maisha yake ,  aliamini ugumu wa maisha  ni moja ya changamoto  katika maisha yangu na kuwa na imani ya kutafuta  kwa juhudi kujikwamua katika hali hii ya umasikini na kumlea mama yangu vizuri, maana mimi ndiye mtoto pekee inabidi nipambane  kwa uwezo wangu wote” ( Hamady aliwaza pindi anapobeba gunia la nyanya akiwa anapeleka Sokoni).  Kwa kweli Hamady ni kijana anayejituma sana tena kwa uchungu kwa sababu  maisha yake ni magumu na pia jicho lake likiwa linamtazama kwa mama yake kwa kuwa anampenda sana. Mungu anamsaidia Hamady kwa kumlinda wakati anaanza kazi mpaka pale anapomaliza kwa usalama.  Baada ya kumaliza kazi huwa anajiandaa kwa kurudi nyumbani,   kwa kawaida baada ya kazi  kufanya  manunuzi  ya mahitaji yote ya nyumbani  ndipo anachukuwa gari la Kariakoo kuelekea Kimara,  wakati yupo kwenye daladala bado anaonekana mwenye  mawazo sana “lini itakuwa furaha kwake kwa kuyashinda maisha haya magumu ya umaskini  ili amlee mama yake? ”  (alijiuliza  maswali mengi wakati yupo kwenye daladala).  Aliwahi kufika kituoni Kimara kwa kuwa hapakuwa na msongamano wa magari barabarani.  Baada ya kuteremka kwenye daladala alijitahidi kutembea kwa haraka ili awahi kufika nyumbani kumwona mama yake kipenzi. Baada ya Hamady  kuwasili nyumbani maandalizi ya chakula yakafanyika,  na  baada ya kumaliza kula akaelekea chumbani  kwake kupumzika huku akifungulia sauti ya redio kwa mbali huku ikimuliwaza  kwa muziki mzuri toka barani Ulaya uliokuwa unakonga moyo wake, Hamady alikuwa anapenda sana muziki na kuimba nyimba za wanamuziki wengi maarufu  na alipenda sana kuimba nyimbo za mwanadada maarufu  Celline Dion.   

Itaendelea jumatatu

Kwa maoni ushauri 0712 592 790 

No comments:

Post a Comment

KATUNI ZA MWAGITO HIZI HAPA MWANANGU.