NA MWANDISHI WETU
MSANII wa Bongo Fleva nchini, Ali Kiba, jana
alisaini mkataba na kampuni kubwa ya muziki ya Sony Music mjini Johannesburg
nchini Afrika Kusini, ambayo itakuwa inamsimamia kazi zake za muziki.
Kazi kubwa itakayokuwa ikifanya kampuni hiyo ni
kusimamia video zake pamoja na audio kwa kuzilipia na kuzifikisha kwenye masoko
makubwa ya muziki duniani.
Baadhi ya wasanii waliochini ya kampuni hiyo ni Davido
ambaye ni msanii wa kwanza kwa Afrika wengine ni Chris Brown na John Legend.
Awali msanii huyo alikuwa na mkataba wa muda na
Kampuni ya One 8 ya nchini Marekani, mbayo haikudumu ingawa aliimba wimbo na
mkali wa muziki R. Kelly.
No comments:
Post a Comment