Wednesday, July 1, 2015

HADITHI

ILIPOISHIA JUMATANO:
“naongea na nani mwenzangu…….???”mdogo wake Mr.Ngowi aitwaye Paulo akauliza
“unaongea na Daktari mkuu kutokea T.M.J hospital”daktari akajibu
Ikabidi Paulo anyanyuke aliko kuwa ameketi na kusogea pembeni kidogo kwa lengo la kuzungumza vizuri na Daktari.

SASA ENDELEA
“okay nakusikiliza “
“sisi wanaume tumepewa moyo wa uvumilivu kwa kila jambo,kitu ninacho kwambia naomba ujikaze kama mwaume sawa…..??”Daktari akamuuliza Paulo kama anaweza kuvumilia kupokea ujumbe mzito kuhusu kifo cha kaka yake.
“sawa nakuhaidi nitavumilia”Paulo akajibu akiwa amejawa na hofu kubwa moyoni mwake pia kichwa kikiwa kimejawa na maswali mengi yaliyo kosa majibu kwa muda mchache.
“kaka yako Mr.ngowi ametutoka atunaye tena dunia kuanzia sasa pole sana ndugu yangu”
“sawa nimekuelewa “Paulo akajibu kwa unyonge huku machozi yakiwa yanamtiririka.
“pole sana nakuomba ufike hapa hospital hili uchukue baadhi ya vitu vya muhimu alivyo kuwa acha marehemu”Daktari baada ya kusitisha mazungumzo Paulo aligundua taarifa hiyo ya kifo cha kaka yake imemuhuzunisha sana, akutaka kabisa kumueleza taarifa nyingine ya huzuni kuhusu shemeji yake mke wa Mr.Ngowi mpaka pale atakapofika hospital.
“okay Daktari hiyo hospitali ya T.M.J iko sehemu hapa Dar es salaam……..??”Paulo akamuuliza Daktari hili amuelekeze .Jmaana akuwa anapafahamu T.M.J hospital.
“sawa T.M.J hospital ipo mikocheni Kawawa road,inatazamana na Mayfair Plaza”Daktari akamjibu “okay Daktari hiyo hospitali ya T.M.J iko sehemu hapa Dar es salaam……..??”Paulo akamuuliza Daktari hili amuelekeze maana akuwa anapafahamu T.M.J hospital.

            Paulo aliumia sana baada ya kupata taarifa ya kifo cha kaka yake aliyekuwa anamtegemea kwa msahada mkubwa,alishindwa kuamini asilimia mia mpaka pale atakapo fika hospital na kuuona mwili wa kaka yake, kwa kuwa muda wa masaa matatu yaliyo pita walikuwa pamoja maeneo wakijadili mambo ya kukuza kampuni zao mpya walizo fungua hili wapate faida nzuri ikiwezekana miaka kazaa ijayo wawe na miladi nje ya mipaka ya Tanzania nchi jirani kama Malawi,Zimbabwe,Uganda na Kenya lakini mipango ya mungu aina makosa maana sisi tunapanga Mungu utimiza aina namna tushukuru kwa yote ndiyo kauli aliyo jifaliji nayo Paulo akatoa simu yake ya kiganjani aliyoweka kwenye mfuko wa shati na kutafuta namba ya shemeji yake mke wa Mr.Ngowi baada ya kuipata akampigia lakini ikawa haipatikani.Paulo alizidi kuchanganikiwa ikabidi atoke nje na kutuacha sisi tunacheza game ya magari iitwayo play station, bila kutambua chochote kinachoendelea kuhusu wazazi wetu.Baada ya Paulo kutoka nje akamuita mlinzi na kumueleza kila kitu kinachoendelea kuhusu kifo cha Mr.Ngowi lakini Paulo akataka mlinzi aonyeshe hali yoyote hili watoto wasielewe kinachoendelea mpaka pale watapokuwa wamefika hospital na kupata uwakika.mlinzi aitwae John akafungua geti,ikabidi Paulo aingie ndani ya gari na kuelekea hospital bila ya kutuaga kwa kuwa akutaka sisi tufahamu chochote kinachoendelea,kila wakati Paulo alipokuwa anaendesha gari akajaribu kumpigia shemeji yake katika simu yake ya kiganjani lakini akufanikiwa kumpata kabisa alizidi kupatwa na hofu zaidi,kwa kuwa barabarani hapakuwa na msongamano wa gari kabisa ikasadia Paulo kufika kwa haraka hospital akapaki gari vizuri akashuka na kuingia hospital kabla ya kumpigia Daktari aliyempatia taarifa ya kifo cha kaka akampigia tena shemeji yake lakini bado simu yake ya kiganjani ikawa haipatikani, Paulo akampigia Daktari mkuu aliyempatia taarifa simu ikaita kwa muda na kupokelewa.

“helooo…Daktari nimeshafika hapa T.M.J hospital”
“okay uko wapi”Daktari akamuuliza Paulo.
“nipo hapa mapokezi “Paulo akajibu
“okay panda lifti njoo ghorofa ya tatu wodi namba 16”
“sawa Daktari nakuja”
          Paulo akasogea hatua chache kutoka pale alipo kuwa mpaka palipokuwa na lifti,akabonya kitufe kati ya vitatu vilivyokuwa na alama tofauti tofauti atimaye lifti ikafunguka na Paulo akaingia ndani na kuelekea ghorofa ya tatu,baada ya kufika akatoka kwenye lifti na kuanza kutizama avijibao vidogo vidogo vilivyo kuwa kwenye kila wodi na kuandika namba za wodi,macho ya Paulo yalitizama huku na kule mwishowe akakutana na wodi namba16.
           Akasukuma mlango na kuingia wodini,alipo ingia ndani akakutana na Daktari mkuu akiwa na Manesi wawili wakiwa wametawaliwa na huzuni kwenye huzuni Paulo baada ya kutizama kitandani akakutana na sura ya kaka yake akiwa amelala kitandani amewekwa pamba masikioni na mdomoni kwa haraka akuweza kuamini ikabidi asogee taratibu mpaka kitandani alipolala kaka yake huku machozi ya uchungu yakiwa yanamtiririka, akamgusa kaka yake huku akiwa analia kwa uchungu sana Daktari na Manesi wakamshika Paulo na kumbembeleza na kumliwaza,baada muda mchache wakaingia Madaktari wanne wakaufunika vizuri mwili wa Mr.Ngowi na kuutoa katika 

ITAENDELEA JUMATANO

No comments:

Post a Comment

KATUNI ZA MWAGITO HIZI HAPA MWANANGU.