Wednesday, April 23, 2014

Mbozi wasaka vipaji

Na Ihola Mwasandube
UONGOZI wa timu ya mpira wa wavu ya Mbozi iliyopo mkoani Mbeya, umeanza mkakati wa kusaka vipaji katika  shule za msingi wilayani humo.

Akizungumza na KAMANYANI.COM kwa njia ya simu jana, meneja wa timu hiyo, Callyxtus Mponzi, aliweka wazi dhamira yao ya kusaka vipaji shuleni kuwa ni kuupa mchezo huo nafasi ya kujulikana na jamii kirahisi kupitia wanafunzi.

"Kwa sasa mchezo huu umeanza kupata mwamko katika wilaya ya Mbozi, tofauti na ilivyokuwa awali, ambako tulikuwa watu wachache katika timu hii," alisema.

Mbali na hilo, Mponzi alisema timu hiyo waliianzisha mwaka 2010, ambapo ilikuwa kama ya mazoezi ya kujifurahisha, lakini baada ya muda wakaanza kushiriki katika mashindano mbalimbali na hadi walipofikia kupanua wigo kuona wanafika mbali zaidi.


No comments:

Post a Comment

KATUNI ZA MWAGITO HIZI HAPA MWANANGU.