Mjeda mmoja jina tunalo hivi majuzi aliamua
kutembeza kichapo kwa mke wa mtu baada ya kuitwa akaamue ugomvi ulikowa
ukiendelea baina ya wanandoa wawili huko Changanyikeni Shuleni jijini Dar.
Akiongea kwa uchungu na jazba mwanamke huyo anayedai
kutembezewa kichapo hicho na mjeda huyo alisema mwanajeshi huyo ambaye ni
jirani yao aliitwa nyumbani kwao hapo kwa ajili ya kuamulia ugomvi uliokuwa
ukiendelea baina yake na mumewe lakini cha kustaajabisha badala ya kufanya kazi
iliyomleta yeye alifika na kuanza kutembeza kichapo cha nguvu kilichopelekea
mwanamke huyo kupata maumivu makali sehemu ya kifuani.
Sakata hilo
lililotokea maeneo ya Changanyikeni juu Shuleni lilimalizika mnamo saa sita
usiku baada ya majirani kadhaa kumpeleka mama huyo kwa mjumbe ambaye aliamuru
waende polisi au wakayamalizie nyumbani angalia picha za tukio zima hapa.
Mume wa mama huyu pichani akimpoza mkewe na jirani yao mmoja jana usiku.
presha imepanda sasa
No comments:
Post a Comment