Timu ya soka ya New Habari inayo milikiwa na kampuni ya New
abari (2006) Limited ijumaa hii inatarajia kujitupa uwanjani kwaajili ya
mtanange utakaopigika katika uwanja wa chuo cha Takwimu kilichopo Changanyikeni
jijini Dar.
Mshambuliaji hatari wa New Habari Fc. Shedrack Kilasi (Hicharito)
Akizungumza na KAMANYANI.COM mratibu wa timu hiyo Jonathan
Tito alisema mchezo huo wa kirafiki unatarajia kuwa mgumu kwa upande wao
kutokana na timu yake kuto fanya mazoezi kwa muda mrefu tangu walipomaliza
mashindano ya Nssf mwezi wan ne hata hivyo Tito amesema kuwa timu yake itaibuka
na ushindi kutokana na wachezaji wake baadhi kuwa na mazoezi binafsi na timu
zao za mitaani.
Tito aliwataja baadhi ya wachezaji wanaotarajia kuanza
katika kikosi chake kuwa ni pamoja na Msham Ngojwike,Kulwa Karedia,Mohamed
Mharizo,Idy Suka, pamoja na msambuliaji wao tegemeo Shedrack Kilasi (Chicharito)
pia alisema mechi hiyo ni mwanza tu wa mechi za kirafiki zinazotarajiwa kuwepo
kila juma.
No comments:
Post a Comment