MSANII anayesifika kwa kugawa fedha kwa mashabiki
wake katika baadhi ya maonyesho yake ya kimuziki, Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’, amefunguka kuwa ipo siku tofauti zao
na mkali mwenzake, Abdul Nasib ‘Diamond’ zitakwisha na watafanyakazi kama
zamani.
Akizungumza juzi alipotembelea Ofisi za New Habari
Limited (2006), zinazochapisha magazeti ya Mtanzania, Bingwa, Rai, Dimba na The
African, Ommy D alisema Diamond alikuwa rafiki yake wa karibu tangu zamani na
walikuwa wakifanya kazi pamoja hivyo yaliyotokea ni moja ya mapito katika
maisha ya mwanadamu yeyote.
“Siwezi kuongelea kitu chochote kinacholeta mapito
haya lakini haya ni maisha nafahamu ipo siku tutakaa pamoja na kufanya kazi
tena kama zamani,” alisema.
Dimpoz aliongeza kwamba kilichotokea kati yao kinaweza
kutokea kwa yeyote katika maisha hivyo kinachotakiwa ni kusimama imara na
kupambana na mapito hayo ndiyo maana kwa sasa kila mtu ana muziki wake na
mashabiki wake.
No comments:
Post a Comment