Friday, May 20, 2016

MWALI WA KWANZA AWASILI HISPANI NA SEVILA.


AndalusiA, Hispania
NDEGE ya kukodi iliyowabeba mabingwa wa Ligi ya Europa, Sevilla imewasili jana asubuhi mjini Andalusia, baada ya kuwachapa Liverpool mabao 3-1 katika mchezo wa fainali uliopigwa kwenye Uwanja wa St. Jakob Park mjini Basel, Uswisi.
Kundi la mashabiki lilikuwa likisubiri katika Uwanja wa ndege wa San Pablo na kikosi hicho kilionyesha taji hilo kwa mashabiki wao ambao walijawa na furaha isiyokifani.

Kikosi hicho hakitafanya sherehe hadi watakapocheza fainali ya Kombe la Mfalme dhidi ya Barcelona kwenye Uwanja wa Vicente Calderon, Jumapili hii.

No comments:

Post a Comment

KATUNI ZA MWAGITO HIZI HAPA MWANANGU.